habari za sasa hivi kitaifa,kimataifa,makala,burudanina michezo

Monday, November 10, 2014

Posted by Unknown | 3:42 AM | No comments
MWANAANGA  wa Kijerumani Alexander Gerst anatazamiwa kuwasili katika sayari ya dunia baada ya kuwa katika Kituo cha Anga za juu cha kimataifa kwa miezi sita. Gerst mwenye umri wa miaka 38 amekuwa akionyesha picha alizopiga na wanaanga wenzake na mandhari ya dunia tokea alipowasili katika kituo hicho cha Anga za juu cha Kimataifa ISS hapo mwezi wa Mei.Gerst na wahandisi wenzake Reid Wiseman wa Shirika la Utafiti wa Anga za juu la Marekani NASA na Kamanda Maxim Suraev wa Shirika la Anga la Urusi wanatarajiwa kutuwa nchini Kazakhstan leo hii katika chombo chao cha anga za juu cha Soyuz.

0 comments:

Post a Comment

Bookmark Us

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter