habari za sasa hivi kitaifa,kimataifa,makala,burudanina michezo

Wednesday, November 12, 2014

Posted by Unknown | 5:45 AM | No comments


Wamefariki watu takriban 5,000  Afrika Magharibi kutokana na Ebola
Muuguzi mmoja nchini Mali pamoja na mgonjwa aliyetibiwa na muuguzi huyo wamefariki kutokana na ugonjwa wa Ebola.
Idadi hiyo inafikisha watu watatu waliofariki kutokana na Ugonjwa huo nchini Mali.
Mgonjwa alikuwa mwanamume mganga wa kiisilamu aliyekuwa na umri wa miaka 50 na alikuwa ameingia nchini humo kutoka Guinea.

Alikuwa ametibiwa na muuguzi aliyefariki akiwa na umri wa miaka 25 mjini Bamako katika kliniki ya Pasteur ambayo kwa sasa imekfungwa na kuwekwa karantini.

Vifo hivi havijahusishwa na kifo cha mtoto mwenye umri wa miaka miwili aliyefariki kutokana na Ebola mwezi oKtoba.
Shirika la Afya Duniani limetangaza mlipuko huu wa Ebola kama janga la dunia.



Aliyekuwa wa kwanza kufariki  MALI kutokana na Ebola  ni Mtoto mwenye umri wa miaka miwili


Kesi hii ya Mali imeibuka siku moja baada ya shirika la Afya Duniani kuwatoa watu ishirini na tano karantini waliodhaniwa kumkribia msichana wa miaka miwili aliyefariki Oktoba .
Walikuwa miongoni mwa watu 100 waliokuwa karantini.

Kisa cha mtoto huyo kuugua na kufariki kutokana na Ebola kimewashangaza sana maafisa wakuu kwani inaarifiwa alisafiri kwa basi kutoka Guinea kuja Mali.

Takriban watu 5,000 wamefariki kutokana na Ebola katika mataifa ya Afrika Magharibi hasa nchini Guinea, Liberia na Sierra Leone.

0 comments:

Post a Comment

Bookmark Us

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter