habari za sasa hivi kitaifa,kimataifa,makala,burudanina michezo

Tuesday, December 9, 2014

Posted by AMMY YEYOO | 5:53 AM | No comments
Dar es Salaam.

Mtu mmoja anayesadikiwa kuwa ni daktari feki amekamatwa katika Hospitali ya Muhimbili, kitengo cha Moi akiwa na vifaa mbalimbali vya kitabibu, ikiwamo majina ya dawa zinazotumika wakati na baada ya kutoa mimba.
Daktari huyo feki alikamatwa jana saa 3.00 asubuhi akiwa amevalia koti la kidaktari ndani ya majengo ya hospitali hiyo.
Kaimu Ofisa Uhusiano wa Moi, Frank Matua alisema mtu huyo aliyetambulika kwa jina la Dismas John amedaiwa kuwatapeli wagonjwa hospitalini hapo kwa kujifanya daktari anayeweza kuwasaidia kwa haraka na kuwalipisha fedha.
Alisema kabla ya kukamatwa Dismas alikuwa katika harakati za kuwatapeli wafanyakazi wa Moi kwa kutembeza karatasi ya mchango akidai amefiwa na mkewe.
Matua alisema walipompekua walimkuta akiwa na mipira ya mikono inayotumiwa na madaktari, karatasi yenye majina ya dawa nyingi za kutolea mimba, kitabu cha mwongozo kitakachotumiwa na madaktari wa wanawake na kitambulisho cha kupigia kura.
“Inaonekana amebobea katika masuala ya utaoji mimba kwa vitu alivyokutwa navyo lazima awe anajihusisha na vitendo hivyo,” alisema.
Alisema baada ya kukamatwa, daktari huyo feki alipelekwa katika Kituo cha Polisi Selander Bridge kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.
Gazeti hili lilimtafuta kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki kuzungumzia suala hilo, lakini alijibu kupitia ujumbe mfupi kuwa yuko katika kikao.
Hospitali ya Muhimbili licha ya kuwa na utaratibu wa kutumia vitambulisho kwa wafanyakazi wake, bado tatizo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Hili ni tukio la nne kutokea katika hospitali hiyo.

Monday, December 8, 2014

Posted by Unknown | 8:59 PM | No comments






Rais wa kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Tanzania bara leo inaadhimisha miaka 53 toka ilipojipatia uhuru toka kwa Muingereza Desemba 9, mwaka 1961.
Maadhimisho haya ya 53 ni muhimu kwa Watanzania, kutokana na kwamba nchi ipo katika kipindi cha uchaguzi, ambapo Watanzania siku ya Jumapili Desemba 14, watapiga kura, katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji.

Uchaguzi huo ni muhimu, kutokana na viongozi katika ngazi hiyo kuwa karibu kabisa na jamii.
Tanzania pia inaadhimisha miaka 53 ya uhuru wake ikiwa katika harakati za uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge unaotarajiwa kufanyika mwakani.

Ni miaka 53 tangu Tanzania ijipatie uhuru wake, lakini hali za Watanzania wengi bado ni duni, kiuchumi na kijamii.
Posted by Unknown | 7:38 PM | No comments

Bi.Valerie Amos mkuu wa kitengo cha misaada wa umoja wa Mataifa
     

Mkuu wa kitengo cha misaada cha Umoja wa Mataifa Valerie Amos ,amesema kwamba hali ya sasa nchini Syria ni doa katika jamii ya kimataifa,ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa mkakati mkubwa wa misaada ya kibinadamu kuwahi kutokea.

Bi Valie Amos amesema kwamba zaidi ya dola milioni kumi na sita zinahitajika kusaidia harakati za Umoja wa mataifa duniani kwa mwaka ujao,na nusu ya fedha hiyo inahitajika nchini Syria pekee.

Umoja huo umesema kwamba wa Syria wapatao milioni tatu wameikimbia nchi yao kufuatia mapigano yanayoendelea na kukimbilia nchi jirani na wengine milioni kumi na mbili wenye uhitaji wakiwa wametawanyika nchini humo.

Juma lililopita kitengo cha chakula cha umoja huo,kililazimika kupunguza kiwango cha misaada ya chakula kwa wakimbizi wa Syria kutokana na ukosefu wa misaada ya kibinadamu.

Inaarifiwa kwamba kiasi cha dola za kimarekani bilioni kumi na tatu kilichoombwa na umoja wa Mataifa kwa mwaka huu wa 2014 hawakupewa zote.

Monday, November 17, 2014

Posted by AMMY YEYOO | 10:42 PM | No comments
Mahakama ya kijeshi Mashariki mwa Jamuhuri ya Demokrasi ya Congo imemhukumu kifo Kanali Birocho Nzanzu baada ya kubainika na makosa ya kutaka kumuua afisa wa jeshi la nchi hiyo aliyekuwa mstari wa mbele kutokomeza wapiganaji wa M23.Kanal Mamadou Ndala anayedaiwa kuuawa na njama za Kanal Birocho Nzanzu
Waaandamaji wakipinga kuuawa kwa Kanal Ndala
Afisa anayedaiwa kupangiwa njama za kuuawa ni Mamadou Ndala mabaye kwa kiasi kikubwa aliamini katika vita dhidi ya kundi hilo la wapiganaji na ambaye aliuawa mwezi januari mwaka huu.

Mahakama imebainisha kuwa Kanali Nzanzu amekuwa akitumiwa na waasi wa ADF kutoka Uganda kuandaa maujaji.
Posted by AMMY YEYOO | 10:36 PM | No comments

Msanii Mrusi aliyecheza katika filamu mashuhuri ya 'Burnt by the Sun 2', alipoteza uume wake baada ya kujikata akitaka kuwa mwanamke.
Kikubwa kilichomfanya msanii huyo Evgniv Sapaev kujitaka sehemu zake za siri ni kwamba alitaka sana kuwa mwanamke.
Mwanamume huyo alionekana akotoka nje ya nyiumba yake huku damu ikimwagika kutoka kwa sehemu zak nyeti kufuatia upasuaji aliojifanyia mwenyewe.
Msanii huyo mwenye umri wa miaka 38 ambaye nyota yake ilikuwa inang'ara sana alikimbizwa hospitalini kwa huduma ya dharura kwa hofu ya hali yake kuwa mbaya .
Madaktari walijaribu kumshona lakini hawakufanikiwa katika juhudi zao za kumrejeshea mwanamume huyo uume wake.
Afisaa mmoja hospitalini ambako muigizaji huyo alipokea matibabu alisema alikuwa na bahati sana kuponea kwani alivuja damu nyingi na kwamba angepoteza muda kidogo tu angefariki.
Kwa mujibu wa jarida la Mirror, jirani ya Evgniv Sapaev, Arkhip Tikhonov mwenye umri wa miaka 57 alishtuka sana alipombishia mlango na kujionea hali yake akiwa tayari ameanza kudhoofika kwani alikuwa amepoteza damu nyingi sana.
''Alionekana akitisha sana akiwa na damu mikononi mwake huku akishika sehemu yake ya uuma ambayo alikuwa ameikata. Nilidhani alikuwa anafanya mazoezi ya uigizaji, lakini alipozirai mlangoni huku akiwa ameshika sehemu yake ya siri mkooni ndipo nilipogudnua kuwa mambo yalikuwa mbaya,'' alisema jirani wa Evgniv
Baada yua kupata nafuu mwathiriwa alinukuliwa akisema, ''tangu niwe mtoto mdogo nimekuwa nikijihisi kuwa mwanamke. Nilijaribu mara nne kukata nyeti zangu lakini wakati wote sikuwa na ujasiri wa kufanya hivyo.Lakini wakati huu niliweza kufanya hivyo baada ya kumeza tembe za kuzuia maumivu, na kujitaka kwa kutumia kisu.

PAY-Actor-Evgeniv-Sapaev
Badhi walimkosoa msanii huyo kuwa kujikata sehemu zake za isiri badala ya kwenda hospitalini kwa upasuaji.


SOURCE;BBC

Sunday, November 16, 2014

Posted by AMMY YEYOO | 2:10 AM | No comments

bow-wow-keshia-chante
Watangazaji wa kipindi cha 106 & Park Bow Wow na Keshia Chanté
Baada ya miaka 14 ya kuwa hewani, kipindi maarufu cha 106 & Park cha BET kitasitishwa. 

Bow Wow na Keshia Chanté watafanya show ya mwisho, December 19, imetangazwa jana.
Kipindi hicho kilianzishwa mwaka 2000 na watangazaji Free na AJ na mwaka 2006 Terrence J na Rocsi Diaz walikishika.

Hata hivyo mwaka 2015 kipindi hicho kinatarajiwa kupelekwa digital zaidi na kitakuwa kikionekana kupitia BET.com na kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii.
Watangazaji wa kipindi cha 106 & Park Bow Wow na Keshia Chanté
Baada ya miaka 14 ya kuwa hewani, kipindi maarufu cha 106 & Park cha BET kitasitishwa.
Bow Wow na Keshia Chanté watafanya show ya mwisho, December 19, imetangazwa jana.
Kipindi hicho kilianzishwa mwaka 2000 na watangazaji Free na AJ na mwaka 2006 Terrence J na Rocsi Diaz walikishika.
Hata hivyo mwaka 2015 kipindi hicho kinatarajiwa kupelekwa digital zaidi na kitakuwa kikionekana kupitia BET.com na kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Friday, November 14, 2014

Posted by AMMY YEYOO | 12:56 AM | No comments

t1Watu wawili ambao wanashilikilia rekodi ya mtu mrefu zaidi duniani na mtu mfupi zaidi duniani walikutana kwa mara ya kwanza kwenye maadhimisho ya ‘Guinness World...Record Day’ huko London, Uingereza Nov.13.Mtu mwenye urefu zaidi duniani anaitwa Sultan Kösen kutoka uturuki ana urefu wa futi 8, huku mtu mfupi zaidi aitwaye Chandra Dangi kutoka Nepal ana urefu wa inchi 21.5.
t3

t4
t6
t5
t2

Thursday, November 13, 2014

Posted by AMMY YEYOO | 10:02 PM | No comments

Mazishi ya msanii Geez Mabovu ambaye alikuwa maarufu kwenye muziki wa Hiphop Tanzania, yamefanyika leo nyumbani kwao Iringa katika makaburi ya Mlolo.
Mabovu amefariki dunia kwenye hospitali alikokua amelazwa nyumbani kwao Iringa alikokwenda wiki mbili zilizopita kutokea Dar es salaam akisumbuliwa na maradhi ya kifua.
Ndugu, jamaa marafiki, wasanii na watu mbalimbali wamejitokeza kushiriki katika mazishi hayo
image-13-11-14-06-32-2Hizi ni baadhi ya picha za mazishi ya msaniihuyo.
IMG_3073
IMG_3076

IMG_3081
Msafara wa Mazishi

image-13-11-14-06-32-3
image-13-11-14-06-32

Kaburi
Marafiki Mazishi
image-13-11-14-06-32-1
Baba wa Geez
Posted by AMMY YEYOO | 9:53 PM | No comments
BAADA ya kutoka na ngoma nakula ujana ney wa mitego atoka na akadumba

Bookmark Us

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter