habari za sasa hivi kitaifa,kimataifa,makala,burudanina michezo

Tuesday, December 9, 2014

Posted by AMMY YEYOO | 5:53 AM | No comments
Dar es Salaam.

Mtu mmoja anayesadikiwa kuwa ni daktari feki amekamatwa katika Hospitali ya Muhimbili, kitengo cha Moi akiwa na vifaa mbalimbali vya kitabibu, ikiwamo majina ya dawa zinazotumika wakati na baada ya kutoa mimba.
Daktari huyo feki alikamatwa jana saa 3.00 asubuhi akiwa amevalia koti la kidaktari ndani ya majengo ya hospitali hiyo.
Kaimu Ofisa Uhusiano wa Moi, Frank Matua alisema mtu huyo aliyetambulika kwa jina la Dismas John amedaiwa kuwatapeli wagonjwa hospitalini hapo kwa kujifanya daktari anayeweza kuwasaidia kwa haraka na kuwalipisha fedha.
Alisema kabla ya kukamatwa Dismas alikuwa katika harakati za kuwatapeli wafanyakazi wa Moi kwa kutembeza karatasi ya mchango akidai amefiwa na mkewe.
Matua alisema walipompekua walimkuta akiwa na mipira ya mikono inayotumiwa na madaktari, karatasi yenye majina ya dawa nyingi za kutolea mimba, kitabu cha mwongozo kitakachotumiwa na madaktari wa wanawake na kitambulisho cha kupigia kura.
“Inaonekana amebobea katika masuala ya utaoji mimba kwa vitu alivyokutwa navyo lazima awe anajihusisha na vitendo hivyo,” alisema.
Alisema baada ya kukamatwa, daktari huyo feki alipelekwa katika Kituo cha Polisi Selander Bridge kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.
Gazeti hili lilimtafuta kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki kuzungumzia suala hilo, lakini alijibu kupitia ujumbe mfupi kuwa yuko katika kikao.
Hospitali ya Muhimbili licha ya kuwa na utaratibu wa kutumia vitambulisho kwa wafanyakazi wake, bado tatizo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Hili ni tukio la nne kutokea katika hospitali hiyo.

0 comments:

Post a Comment

Bookmark Us

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter